love_story_25774529.jpgNatumai utakuwa u mzima wa afya kabisa. Kama ilivyo matatizo mengine tatizo la kukosa hamu ya kushiriki tendo la ndoa huwakumba na wanaume vilevile ila siyo kwa kiwango kikubwa sana kama ilivyo kwa wanawake.
Katika makala haya tutaaangalia kwa kina sababu za tatizo hili kwa wanaume na athari zake na mwisho tutajifunza njia za kutatua au kuondokana na tatizo hili.
Mwili wa mwanadamu uliumbwa ukiwa na matamanio na si mbaya kama mwenye mwili atakuwa na uwezo wa kujitawala. Wanaume wengi huvutiwa zaidi na hisia za kushiriki tendo kwa kuona baadhi ya maungo ya wanawake, kusikia sauti na hata migusano.
Kuna wanaume wengi wao wapo tu siku zinaenda hawapati hamu ya kushiriki tendo la ndoa na wanajiona kama ndiyo wamefanikiwa kujitawala kumbe ni wagonjwa.
Habari njema ni kwamba pamoja na tatizo hili kuwasumbua watu wengi kuna mambo unayoweza kuyafanya kupunguza ukubwa wa tatizo hili au kuliondoa kabisa, kwa kutumia mimea tiba na matunda tiba.
Unachotakiwa kufanya kama umejaribu kutumia njia mbalimbali ili kuondoa tatizo hili bila mafanikio basi wahi mapema kwa wataalamu ufanyiwe uchunguzi au ukatutembelea Sigwa Herbal Clinic tukakusaidia kuliondoa kabisa tatizo hilo na ukarejea katika hali ya kawaida. Baadhi ya watu wanaamini kuwa hamu ya kufanya tendo la ndoa inapungua kadiri umri wa mwanaume unavyoongezeka. Kuna idadi kubwa tu ya wanaume ambao hamu yao ya kufanya tendo la ndoa imebaki vilevile hata umri wao ulipokuwa mkubwa kabisa. Kwanza tuanze kwa kutazama ukubwa wa tatizo hili.
Idadi ya wanaume wanaoridhika kuishi na tatizo hili ni ndogo sana ukilinganisha na ile ya wanawake.
Hata hivyo, tatizo la mwanaume kukosa hamu ya kushiriki tendo limekuwa ni chanzo kikubwa katika kuleta migogoro katika ndoa nyingi.
Wanaume kwa kawaida ni wabishi sana na huwa hawapendi kuaibika hivyo mtu anaweza akawa na tatizo ila hapendi mwenzi wake ajue kama ana tatizo ambalo kumbe angeliweka bayana angepata ushauri wa namna ya kulitatua.
Pamoja na kwamba tatizo hili halijitokezi sana kwa wanaume ukilinganisha na wanawake, inakadiriwa kuwa asilimia 15 hadi 16 ya wanaume wana tatizo hili, ni sawa na uwiano wa mwanamme mmoja mwenye tatizo hili katika kila wanaume sita au saba. Idadi ya wanawake wenye tatizo hili ni mara mbili ya wanaume.
Tatizo hili huwakera zaidi wanaume kuliko wanawake kwa sababu wanaume huchukulia urijali kama sehemu ya ukamilifu wa mwanamme na hukosa raha wanapoona wana mapungufu kuhusu mambo ya mapenzi, tofauti kabisa na wanawake.
Natumai utakuwa u mzima wa afya kabisa. Wiki iliyo pita tulianza kuaangalia sababu zinazopelekea wanaume kukosa hamu ya kushiriki tendo la ndoa na mwenza wake.Kama nilivyoeleza wiki iliyopita ni kwamba; katika Makala haya tutaaangalia kwa kina sababu za tatizo hili kwa wanaume na athari zake na mwisho tutajifunza njia za kutatua au kuondokana na tatizo hili.
Leo tutaangalia sababu au vyanzo vinavyopelekea mwanaume kukumbwa na tatizo hili la kukosa hamu ya kushiri tendo la ndoa.
Tatizo la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa kwa mwanaume linaweza kusababishwa na vitu vingi sana.
Sababu hizo zinaweza kuwa za kimaumbile au kisaikolojia au za mchanganyiko wa vitu hivyo viwili. Hebu tuone baadhi ya vyanzo vya tatizo hili.
Mahusiano Baina Ya Mwanaume Na Mwanamke
Uhusiano kati ya mwanume na mwanamke ambao ni wanandoa una mchango mkubwa katika kujenga au kubomoa matamanio ya mwanaume.
Kama kutakuwa na matatizo ya mahusiano kati ya mwanaume na mwanamke yana mchango mkubwa sana katika kusababisha tatizo la kukosa hamu ya mapenzi.
Ni vema ukajihoji kama mahusiano yako na mwenza wako yapo sawa. Na mara nyingine unaweza ukawa umekuwa katika mahusiano kwa mda mrefu kiasi ambacho umemzoea hali inayopelekea kukosa hamu ya kushiriki nae tendo la ndoa. Hili nalo hutokea mara nyingi.
Matumizi Ya Madawa Na Pombe
Matumizi ya baadhi ya madawa na unywaji wa pombe wa kupindukia huweza kuleta tatizo hili la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa. Madawa yanayochangia tatizo hili ni pamoja na;Madawa ya high blood pressure, Madawa ya kuondoa msongo wa mawazo, Madawa yote yanayozuia ufanyaji kazi au uzalishaji wa testosterone, kwa mfano, cimetidine, finasteride na cyproterone.
Matatizo Katika Mfumo Wa Homoni
Tumeshaona kwamba upungufu wa homoni inayoitwa testosterone unasababisha kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa. Matatizo mengine katika mfumo wa homoni huchangia tatizo hili.
Kama thyroid haitoi homoni za kutosha, tatizo hili huweza kutokea ingawa mchango wa thyroid katika tatizo hili ni mdogo sana. Thyroid ni kiungo cha kuzalisha homoni kilichopo katika eneo la shingo.
Umri Kuwa Mkubwa
Kiwango cha testosterone katika mwili wa mwanaume hupungua kwa asilimia 1-2 kila mwaka kadri mwanaume anvyozidi kuwa na umri mkubwa. Homoni ya msingi sana kuhusiana na masuala ya mapenzi huitwa testosterone. Kwa mwanaume homoni hii hutolewa kwa kiwango kikubwa na korodani na kwa mwanamke hutolewa na ovari.
Homoni ikipungua katika mwili wa binadamu, humfanya apoteze hamu ya kufanya tendo la ndoa.  Kiwango cha testosterone kikishuka sana katika mwili wa mwanaume huyu humfanya asiwe na nguvu, ashindwe kutuliza mawazo kwenye jambo alifanyalo na apoteze hamu ya kufanya mapenzi.
Natumai utakuwa u mzima wa afya kabisa. Wiki iliyo pita tulianza kuaangalia sababu zinazopelekea mwanaume kukosa hamu ya kushiriki tendo la ndoa na mwenza wake. Kama nilivyoeleza wiki iliyopita ni kwamba; katika Makala haya tutaaangalia kwa kina sababu za tatizo hili kwa wanaume na athari zake na mwisho tutajifunza njia za kutatua au kuondokana na tatizo hili.
Tatizo la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa kwa mwanaume linaweza kusababishwa na vitu vingi sana.  Nikukumbushe tu kwamba sababu hizo zinaweza kuwa za kimaumbile au kisaikolojia au za mchanganyiko wa vitu hivyo viwili. Fuatilia kwa makini;
Uchovu.
Wakati mwingine uchovu hupelekea mtu kukosa hamu ya kushiriki tendo la ndoa. Na ikiwa mtu atakuwa anasongwa na shughuli nyingi zinazochosha mwili kiendelevu hamu ya kushiriki tendo la ndoa huanza kupungua na ikizidi basi baadaye mwanaume husika atakosa hamu ya kushiriki tendon la ndoa na itahitaji uangalizi mkubwa ili arejee katika hali yake ya kawaida. Vilevile kukosa mpango mzuri wa shughuli zako za kila siku na kujaribu kulazimisha kufanya mapenzi katikati ya ratiba yako iliyojaa. Mahusiano ya kimapenzi yanataka yatengewe muda wake na unaotosha.
 MsongoWa Mawazo
Msongo wa mawazo ni ugonjwa wa hali ya kuwa na mawazo makali ya muda mrefu ya kukukosesha raha hali inayopelekea kushindwa kuyafanya mambo yako ya kawaida kiufanisi.   Mawazo ya namna hii huathiri mwenendo wako wa maisha yako pamoja na matamanio yako ya kimapenzi. Mwanaume anasongwa na mawazo kiasi cha kuathiri katika ufanisi wa shughuli zake anaweza kupoteza hamu ya kushiriki tendo la ndoa.
Kuwahi kufika kileleni
Katika vitu ambavyo wanaume wengi hawapendi vijulikane na wenzi wao ni tatizo la kuwahi kufika kileleni. Kila mwanume hupenda aonekane ni rijali au mwanaume kamili mwenye uwezo wa kushiriki tendo la ndoa bila shida yoyote. Na imezoeleka katika jamii zetu ikiwa mwaume atakuwa ana tatizo la kuwahi kufika kileleni anaweza akatangazwa mtaa mzima kila mtu ajue, hali hii hupelekea aibu kubwa na fedheha.
Katika mazingira kama hayo mwanume mwenye tatizo hilo hata kama hajatangazwa na mwenzi wake amemtunzia siri hiyo, anajihisi kuwa hafai. Hali hii humfanya kila anapopata hamu ya kushiriki tendo la ndoa aogope kushiriki tendon a mwenza wake kwani ataabika. Hii inamchango mkubwa sana katika kumfanya mwanume apoteze hamu ya kushiriki tendo la ndoa.
Tumekuwa tukiangalia tatizo la wanaume wengi kushindwa kushiriki tendo la ndoa. Tumeangalia jinsi tatizo hili linavyoisumbua jamii yetu na pia tumejua kuwa mwanaume kukosa hamu ya kushiriki tendo la ndoa si jambo la kawaida ni tatizo linaloweza kutibika.   Zifuatazo ni njia za kuondoa tatizo la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa
 Wengi wanatarajia kuambiwa wameze dawa fulani ili kuondokana na tatizo hilo. Kama unatatizo hilo ni vema ukawaona matabibu kwa ushauri na uchunguzi ili kujua chanzo cha tatizo na upate matibabu. Ni vema kwa wanaume wenye tatizo hilo washirikiane na wake zao ili kuliondoa tatizo hilo.
Katika nchi zilizoendelea, wataalam wamekuwa wakigundua dawa na vifaa tiba vipya vya kuondoa tatizo hili na vingi bado ni vya bei kubwa na/au vinapatikana kwa shida. Vipo ambavyo vimeonyesha mafanikio makubwa, mifano ya vitu hivyo ni Suction Vibrators, Desire Creams na Erection Drugs. Habari njema ni kwamba tatizo hili linaweza kutatuliwa kwa mimea tiba na matunda tiba ya kawaida ambayo ipo katika mazingira yetu yanayotuzunguka.
Utafiti umeonyesha kuwa tunachokula ndicho kinachotujenga na kutufanya tuwe watu wa aina gani. Vyakula tunavyokula vina mchango mkubwa katika kujenga au kubomoa afya zetu hivyo nimuhimu kuwa makini katika kuamua tule nini na tunywe nini. Kuna uhusiano mkubwa kati ya chakula tunachokula na afya ya viungo vya uzazi. Baadhi ya chakula na virutubisho vimehusishwa na hamu ya kushiriki tendo la ndoa.
Virutubisho ndani ya chakula ambavyo vinasaidia hali hiyo ni antioxidants, vitamin C, vitamin E, potassium na zinc. Kirutubisho cha zinc kinaongeza mbegu kwa mwanamme (sperm count) hivyo humsaidia kuongeza hamu ya kufanya tendo la ndoa. Chakula cho chote chenye virutubisho hivi vikiliwa humfanya mlaji asikie hamu ya kushiriki tendo la ndoa.
Baadhi ya vyakula kula na matunda tiba hayo ni kama vile:
Tikitimaji-Hili linachukuliwa kuwa ndilo tunda bora katika kuboresha afya ya mapenzi. Tunda hili lina asilimia 92 ya maji na asilimia 8 zinazobakia zina phytonutrient citrulline ambayo hugeuzwa kuwa arginine. Arginine ni amino acid ambayo hufanya mishipa ya damu kuwa kwenye hali ya ubora wake na kusadia damu kupita vizuri zaidi. Tikitimaji kwa hiyo husaidia damu ifike kwa kiwango kizuri zaidi kwenye sehemu ambazo hutakiwa kutanuka wakati mtu akipata hisia za kufanya tendo la ndoa ambazo ni viungo vya ndani ya kisimi cha mwanamke na ndani ya uume wa mwanamme.
Parachichi -Tunda hili lina vitamini E ambayo ni antioxidant. Ndani ya tunda hili kuna potassium na vitamini B6 ambavyo huboresha afya ya moyo na kusaidia mzunguko wa damu.
Strawberries–Tunda hililina antioxidants kwa kusaidia afya ya moyo na mishipa ya damu (arteri) na vitamin C ambayo huongeza kiwango cha mbegu kwa mwanaume.
Kuna mchanganyiko wa matunda ukisagwa pamoja na kunywewa umeonyesha kuongeza hamu ya kushiriki tendo la ndoa.   Kwa ziada unaweza kutumia karafuu, mayai na tangawizi pia.
Nakushauri msomaji wangu ufuatilie kwa makini Makala haya ili kujua vizuri kuhusu tatizo hili. Lakini kama una tatizo hili na unajisikia aibu kumweleza mwenzi wako tupigie simu katika namba zetu au tutembelee Sigwa herbal Clinic katika vituo vyetu vilivyopo Dar es Salaam, Mbeya, Morogoro, Dodoma, Arusha, Tanga, Kigoma, Mwanza.
Nakushauri msomaji wangu ufuatilie kwa makini Makala haya ili kujua vizuri kuhusu tatizo hili. Lakini kama una tatizo hili na unajisikia aibu kumweleza mwenzi wako tupigie simu katika namba zetu au tutembelee Sigwa herbal Clinic katika vituo vyetu vilivyopo Dar es Salaam, Mbeya, Morogoro, Dodoma, Arusha, Tanga, Kigoma, Mwanza.

Post a Comment

Powered by Blogger.