MUNGU akimjalia uhai msanii Bambo, msimu ujao wa uchaguzi mkuu atajitosa miguu yote kuwania udiwani lakini kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Hiyo ni baada ya siku chache zilizopita kujiondoa kwenye kinyang’anyiro hicho cha udiwani wa Kata ya Mchikichini, Ilala alipokuwa anagombea kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM).
Akizungumza na Saluti5 wiki hii, Bambo alisema kuwa, tofauti na mwaka huu, anaamini msimu ujao atakuwa amejipanga kikamilifu pamoja na fursa nzuri ya kuhimili mikiki ya uchaguzi.

Hata hivyo, Bambo hakuweza kuweka wazi sababu inayomfanya aitose CCM na kuhamia CHADEMA katika msimu huo ujao wa kinyang’anyiro cha uchaguzi

Post a Comment

Powered by Blogger.