DSC00994
Katibu wa CCM mkoa wa Singida, Mary Maziku,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) juu ya chama hicho kuhamwa na Mwenyekiti wake wa mkoa, Mgana Izumbe Msindai aliyehamia CHADEMA.(Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
KURA  za maoni nafasi ya udiwani,ubunge wa viti maalum na ule  wa majimbo CCM  mkoani Singida, zimeacha malalamiko na maumivu mengi,ambayo ni pamoja na kuhamwa na wananchama wake wengi akiwemo Mwenyekiti wake wa mkoa, Mgana Izumbe Msindai na Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Ikungi Christina Samwel Hamisi,kujivua uanachama na kujifukuzisha kwenye nafasi zao za  uenyeviti,kwa tuhuma ya kukiuka sheria, taratibu na kanuni.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana,katibu wa CCM mkoa wa Singida,Mary Maziku, alisema Msindai kiongozi wao huyo wa muda mrefu ndani ya chama,hajamjulisha azma yake ya kukihama chama, isipokuwa aliwasiliana na Katibu Msaidizi kuwa mali yake binafsi itolewe kwenye ofisi yake ya CCM.
Alisema CCM mkoa wa Singida kuhamwa na mwenyekiti wake, hakitaterereka hata kidogo na zaidi kitaendelea kusonga mbele ikiwemo kuhakikisha majimbo yote kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu,yanakuwa mikononi mwa CCM.
“Mimi niseme tu kuwa namwombea kila la kheri aliyekuwa Mwenyeiti CCM mkoa na bosi wangu,kwenye safari yake ya kusaka mafanikio makubwa zaidi ambayo ameyakosa ndani ya CCM”,alisema Maziku.
Ingawa haijafahamika hadi sasa, ni nini kimemsibu hadi ahame CCM mahali ambako alipewa cheo kikubwa cha mwenyekiti wa wenyeviti wa mikoa  yote nchini,inadaiwa  ni kutokana na kushindwa kwenye kura za maoni ubunge jimbo la Mkalama,hivi karibuni.
Kwenye kura hizo za maoni,Msindai alikuwa mshindi wa pili kwa kupata kura 3,908 dhidi ya mshindi Allan Joseph Kiula,aliyepata kura 5,823.
Kwa upande wa Mwenyekiti UWT wilaya ya Ikungi,Chrisita,baada ya kushindwa kwenye kura za maoini ubunge viti maalum,siku nne baadaye,alihamia CHADEMA ambapo alichukua fomu kuomba ubunge viti maalum kupitia chama hicho cha upinzani,aliishia kupata kura sifuri (0).
Kwa mujibu wa Katibu Maziku,mwanachama au kiongozi anapohama CCM na kujiunga na chama kingine cha upinzani,automatiki atakuwa amejivua uanachama na nyadhifa zote za uongozi endapo alikuwa nazo.
Katika hatua nyingine, Mwigulu Nchemba, ametetea kwa kishindo nafasi yake ya ubunge wa jimbo la Iramba magharibi kwa kupata kura 25,786 na mpinzani wake David Jairo,akuambulia kura 1,975,Juma Hasan Kilimba (1,827) na Amon Gyuda (236).
Kwa jimbo la Singida mjini liloachwa wazi na Mohammed Gulam Dewji, Maziku alisema kilichotendeka kwenye uchaguzi wa nafasi ya ubunge, imelazimu matokeo yake yatatolewa na katibu mkuu CCM Abrahaman Kinana huko Dodoma siku ambayo hadi sasa haijafahamika.
 Elibariki Emmanuel Kingu,mkuu wa wilaya ya Igunga ameshinda nafasi ya ubunge jimbo la Singida magharibi kwa kupata kura 4,759.Kingu amewahi kuwa mkuu wa wilaya ya Igunga mkoa wa  Tabora.
Wengine na kura zao kwenye mabano,kuwa ni Dinawi Samwel Gabriel (901),Hamisi Shaban Lissu (1,918),Willson Elisha Nkhambaku (2,836),Dk.Hamisi Hema Mahuna (1,013),Dk.Grace Khwaya Puja (762),Yona Daud Makala (252) na Hamisi Hassan Ngila (384).
Kwa upande wa jimbo la Ikungi mashariki,katibu huyo alisema Jonathan Andrew Njau ameshinda kwa kupata kura 6,312 na kufuatiwa kwa mbali na Mdimi Emmanuel Hongoa  aliyepata kura 1,564.
Wengine na  kura zao kwenye mabano kuwa ni  Hamisi Abeil Maulid (1,409),Jacob Theophil Kituu (515),Emmanuel Japhaet Hume (454) na Martin Labia Lissu (1,291).
Katibu wa CCM wilaya ya Manyoni,Dafroza Lucas,alisema nafasi ya ubunge jimbo la Manyoni magharibi,limechukuliwa na mwenyekiti wazazi wilaya ya Manyoni,Yahaya Omari Masare aliyepata kura 6,164 na kufuatiwa na mbunge aliyemaliza muda wake,John Paulo Lwanji,aliyepata kura 2,651.
Dafroza alitaja wagombea wengine na kura zao kwenye mabano kuwa ni Elphas Eammanuel Lwanji (1,387), Jamal Juma Kuwingwa (403),Jane Lucas Likuda (396) Mojammed Juma Makwaya (280),Yohana Stephen Msita (482),Moshi Musa Mmanywa (508),Adimini Mwakapalila (Msokwa (985),Dk.Mwanga Mkayangwa (1,745),Rashid Ramadhani Said (199) na Francis Pius Shaban (80).
Jimbo la Manyoni mashariki,alisema nafasi ya ubunge imechukuliwa na Daniel Edward Mtuka (6,792) akifiatiwa kwa karibu na Dk.Pius Stephen Chaya (6,270).
Dafroza alitaja wengine na kura zao kwenye mabano kuwa ni,Gaitani Francis Romwald (1,542),Joseph Meshack Chitinka (592),AlexNyamejo Manonga (433),Jumanne Bosco Mtemi (715) ,Eng.Horold Jackson Huzi Mtyona (1,212) na Gaitaini Francis Romwald (1,542)

Post a Comment

Powered by Blogger.